banner image

TANZIA

MPOKI BUKUKU
Mpiga picha maarufu Mpoki Bukuku amefariki dunia leo katika Taasisi ya Mifupa (MOI), alikokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.

Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano kwa Umma (MOI) Almas Jumaa.

"Ni kweli Mpoki amefariki dunia mchana huu, alipokelewa jana usiku baada ya kupata ajali ya gari maeneo la Mwenge  ITV, taarifa zaidi tutazitoa baadaye," alisema Almas.

Mpoki Bukuku amewahi kufanya kazi kama Mpiga Picha Mkuu katika gazeti la Mwananchi, linalochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti. Pia amewahi kufanya kazi magazeti kadhaa likiwemo Majira na Nipashe.

 CONVIDA inatoa pole kwa Ndugu na jamaa, kwakumpoteza ndugu yetu Mpoki Bukuku.
Mwenyezi Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya mpendwa wetu. Amen
TANZIA TANZIA Reviewed by CONVIDA FUNERAL HOME COMPANY LIMITED on 1:18 PM Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.