banner image

KWAHERI SIR ANDY CHANDE

SIR ANDY CHANDE


Aliyekuwa Kiongozi wa jumuiya ya Freemason Tanzania na Afrika Mashariki. Sir Jayantilal Keshavji ‘Andy’ Chande amekuwa mwanacham wa Freemason kwa takribani miongo sita tangu ajiunge na umoja huo mwaka 1954.
Kiongozi huyo alizaliwa Mombasa Kenya Mei 7,1928 ingawa wazazi wake walikuwa wakiishi Bukene Mjini mkoani Tabora
Taarifa za kifo chake zilianza kusambaa katika mitandao ya kijamii juziAsubuhi. Kulingana na taarifa hizo kiongozi huyo alifariki dunia jijini Nairobi alikokuwa akitibiwa. Kiongozi huyo anatarajiwa kuchwa jumanne ijayo na kwamba wanataraji zaidi ya watu 300 kutoka nje na ndani ya nchi watahudhuria mazishi yake.
HISTORIA YA SIR CHANDE
Sir Chande alizaliwa Mombasa Kenya Mei 7, 1928, ingawa wazazi wake walikuwa wakiishi Bukene mkoani Tabora magharibi mwa Tanzania.
Alifika Tanzania  mwaka 1950, alihamia Dar es salaam 1953 na kukutana na watu wengi wa bandarini, shirika la reli na mashirika mbalimbali aliyofanyaia kkazi.
Katika simulizi zake kadhaa, Sir Chande alisema alikutana na watu wengi ambao walikuwa wanahudhuria vikao vya Freemason, akaanza kuuliza na akajifunza mambo kadhaa kuhusu watu hao. 
SIR ANDY CHANDE ENZI ZA UHAI WAKE AKIWA NA HAYATI BABA WA TAIFA

Wakati huo, hao watu hawkuwa huru kuzungumzia Freemason kama alivyokfanya Sir Chande, hasa kabla ya vita ya pili ya dunia.
Sir Chande alisema wakati huo Freemason ilikuwa imegawanywa makundi tofauti, katika Hospitali, Shule, na mashirika mbalimbali na kulikuwa na kundi maalum kwa ajili ya matajiri na wanafanyakazi wakubwa wa serikali. Ukiangalia vizuri wengi wao walikuwa ni wazungu na Baadhi ya wahindi.
Kundi la kwanza lilikuwa linaongozwa na watu wa Scotland, makundi mawili yliyofuata yalikuwa yanaongozwa na Waingereza na kundi la nne lilikuwa linaongozwa na wahindi ambalo ndilo Chande alilojiunga nalo. Ilimchukua miaka miwili kukubaliwa kujiunga na Freemason.
Aliapishwa rasmi mwaka 1954 akiwa na umri wamiaka 28. Kumbuka kwamba masharti ya kujiunga ni lazima uwe na umri kuanzia miaka 21.
Baada ya hapo ndipo alipanda cheo nakupewa nafasi ya kuongoza kundi au tawi la Freemason katika nchi za Afrika Mashariki ambazo ni Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda na Burundi.
Akajiunga na miradi tofauti ya Freemason nchini Uingereza yakiwemo hoteli za kifahari pamoja na kupewa jukumu la kujenga hotel mpya ya Freemason nchini Ghana kwenye mji wa Khumasi ambayo ni ya kifahari.
SIR ANDY CHANDE AKIWA NA RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA NNE TZ MHESHIMIWA DR.JK

Hotel nyingine ya kifahari aliyoisimamia ujenzi wake iko Zambia.
Sir Chande anakumbukwa sana kwa kuanzisha shule ya msingi ya viziwi Buguruni, Dar es salaam, moja ya taasisi ambazo alizipa kipaumbele mno hadi anaingia kaburini. Sir Andy Chande alistaafu kama kiongozi wa Freemason Afrika mashariki mwaka 2005 baada ya kuifanyia kazi  kwa miaka 19, akawa hahudhuri mikutano ya nchi hizi lakini akishiriki ile ya Uingereza kwa sababu alikuwa akiendele kufanya kazi huko.

KWAHERI SIR ANDY CHANDE KWAHERI SIR ANDY CHANDE Reviewed by CONVIDA FUNERAL HOME COMPANY LIMITED on 10:14 AM Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.